超碰caoporen国产公开,亚洲男人在线天堂2019香蕉,国产精品对白刺激,九九热这里只有国产中文精品2

China yatafuta na kuipata satalaiti ya kwanza ya majaribio inayoweza kurejeshwa duniani na kutumika tena

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Oktoba 12, 2024

China kwa mafanikio imetafuta na kuipata satalaiti yake ya kwanza ya majaribio inayoweza kurejeshwa duniani na kutumika tena, Shijian-19, kwenye Kituo cha Kutua cha Dongfeng kilichopo Mkoa unaojiendesha wa Mongolia ya Ndani, Kaskazini mwa China saa 4:39 asubuhi (kwa saa za Beijing), Oktoba 11, 2024. (Picha na Wang Heng/Xinhua)

China kwa mafanikio imetafuta na kuipata satalaiti yake ya kwanza ya majaribio inayoweza kurejeshwa duniani na kutumika tena, Shijian-19, kwenye Kituo cha Kutua cha Dongfeng kilichopo Mkoa unaojiendesha wa Mongolia ya Ndani, Kaskazini mwa China saa 4:39 asubuhi (kwa saa za Beijing), Oktoba 11, 2024. (Picha na Wang Heng/Xinhua)

China kwa mafanikio imetafuta na kuipata satalaiti yake ya kwanza ya majaribio inayoweza kurejeshwa duniani na kutumika tena, Shijian-19, kwenye Kituo cha Kutua cha Dongfeng kilichopo Mkoa Unaojiendesha wa Mongolia ya Ndani, Kaskazini mwa China saa 4:39 asubuhi (kwa saa za Beijing) siku ya Ijumaa, limesema Shirika la Anga ya Juu la China (CNSA).

Shirika hilo limesema, vitu vyote vya kurejeshwa kutoka anga ya juu katika nyanja kama vile upandaji, uzalishaji na ukuzaji wa mimea na viumbe vidogovidogo, udhibiti wa kiotomatiki na uthibitishaji wa teknolojia mpya, majaribio ya kisayansi kwenye anga ya juu, pamoja na ustawi wa jamii na uvumbuzi wa kitamaduni, vimeweza kupatikana kwa mafanikio.

Ikiwa ilirushwa Septemba 27 kutoka kwenye Kituo cha Urushaji Satalaiti cha Jiuquan, Kaskazini Magharibi mwa China, Shijian-19 imepata mafaniko kadhaa mapya ya kiteknolojia.

Watafiti walifanya majaribio ya upandaji, uzalishaji, na ukuzaji wa mimea kwenye anga ya juu, uthibitishaji wa teknolojia mpya, na majaribio ya kisayansi kwenye anga ya juu kwa kutumia satalaiti inayoweza kutumika tena, wakilenga kuendeleza maendeleo na matumizi ya teknolojia mpya kuhusu anga ya juu.

Satalaiti hiyo pia ilibeba vitu vingi vya ushirikiano wa kimataifa, ikifanya kazi kama jukwaa bora la kuhimiza ushirikiano wa kimataifa katika utafiti na matumizi ya anga ya juu.

China kwa mafanikio imetafuta na kuipata satalaiti yake ya kwanza ya majaribio inayoweza kurejeshwa duniani na kutumika tena, Shijian-19, kwenye Kituo cha Kutua cha Dongfeng kilichopo Mkoa unaojiendesha wa Mongolia ya Ndani, Kaskazini mwa China saa 4:39 asubuhi (kwa saa za Beijing), Oktoba 11, 2024. (Picha na Wang Heng/Xinhua)

China kwa mafanikio imetafuta na kuipata satalaiti yake ya kwanza ya majaribio inayoweza kurejeshwa duniani na kutumika tena, Shijian-19, kwenye Kituo cha Kutua cha Dongfeng kilichopo Mkoa unaojiendesha wa Mongolia ya Ndani, Kaskazini mwa China saa 4:39 asubuhi (kwa saa za Beijing), Oktoba 11, 2024. (Picha na Wang Heng/Xinhua)

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha