超碰caoporen国产公开,亚洲男人在线天堂2019香蕉,国产精品对白刺激,九九热这里只有国产中文精品2

Kampuni ya China yatia saini mkataba wa kujenga kiwanda cha chanjo dhidi ya kipindupindu nchini Zambia

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Oktoba 09, 2024

Rais Hakainde Hichilema wa Zambia (katikati, nyuma) akishuhudia kusainiwa kwa mkataba wa makubaliano (MoU) kuhusu ujenzi wa kiwanda cha kuzalisha chanjo ya mdomoni dhidi ya kipindupindu nchini Zambia mjini Lusaka, Zambia, Oktoba 7, 2024. (Xinhua/Peng Lijun)

Rais Hakainde Hichilema wa Zambia (katikati, nyuma) akishuhudia kusainiwa kwa mkataba wa makubaliano (MoU) kuhusu ujenzi wa kiwanda cha kuzalisha chanjo ya mdomoni dhidi ya kipindupindu nchini Zambia mjini Lusaka, Zambia, Oktoba 7, 2024. (Xinhua/Peng Lijun)

LUSAKA - Kampuni ya Kimataifa ya Teknolojia za Tiba ya China Jijia, imetia saini Mkataba wa Makubaliano (MoU) na Shirika la Maendeleo ya Viwanda (IDC), shirika la uwekezaji la serikali ya Zambia, kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda cha kuzalisha chanjo ya mdomoni dhidi ya kipindupindu nchini Zambia katika hafla iliyofanyika Ikulu ya Zambia siku ya Jumatatu, ikishuhudiwa na Rais Hakainde Hichilema na Balozi wa China nchini Zambia Han Jing.

Su Yonglin, naibu meneja mkuu wa kampuni hiyo ya China, amesema kampuni hiyo inafurahi kushirikiana na upande wa Zambia kuanza uzalishaji wa chanjo dhidi ya kipindupindu ikiwa ni sehemu ya awamu ya kwanza ya uzalishaji wa nchini humo.

Amesema, kampuni hiyo itaanzisha chanjo pekee dhidi ya kipindupindu ya China, chanjo bunifu cha mdomoni kilichotengenezwa kutoka kwenye utafiti wa Akademia ya Sayansi za Tiba za Kijeshi ya China.

"Utekelezaji wa mradi huu utatoa kinga thabiti ya afya kwa watu wa Zambia, kuongeza ajira za wenyeji, na kuimarisha uwezo wa mwitikio wa dharura wa Zambia katika kukabiliana na janga la afya ya umma," Su amesema.

Rais wa Zambia Hichilema ametoa shukrani kwa mwenzake wa China kwa kufanikisha maono ya Zambia ya kuanza uzalishaji wa chanjo nchini, akisema makubaliano hayo yataifanya Zambia kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kuzalisha chanjo dhidi ya kipindupindu.

"Ushirikiano huu utaokoa maisha, kuongeza nguvukazi, na kutumikia binadamu," amesema.

Amesema, Zambia ilikuwa miongoni mwa nchi zilizo katika hatari kubwa, baada ya kukabiliwa na maambukizi zaidi ya 20,000 ya kipindupindu na vifo karibu 700 wakati wa mlipuko wa Mwaka 2023-2024 na kwamba kiwanda hicho cha chanjo kitahudumia siyo tu Zambia pekee bali pia eneo pana na Afrika nzima.

Kwa upande wake Balozi wa China amesema ubalozi huo utaunga mkono jitihada hiyo kwani chanjo hizo zitasaidia kwa kiasi kikubwa kudhibiti ugonjwa wa kipindupindu nchini Zambia.?

(Wahariri wa tovuti:Song Ge,Zhao Jian)

Picha