超碰caoporen国产公开,亚洲男人在线天堂2019香蕉,国产精品对白刺激,九九热这里只有国产中文精品2

Waangalizi wa amani wa Sudan Kusini waridhia kuongezwa kipindi cha mpito kwa miaka miwili

(CRI Online) Septemba 19, 2024

Tume ya Pamoja ya Ufuatiliaji na Tathmini (RJMEC) imeridhia serikali ya Sudan Kusini kuongeza kipindi cha mpito na kuahirishwa kwa uchaguzi mkuu kwa miaka miwili ili kutekeleza makubaliano ya amani yaliyofufuliwa.

Mwenyekiti wa muda wa tume hiyo Charles Tai Gituai, amesema siku ya Jumatano kwamba uamuzi wa serikali wa kuongeza kipindi cha mpito umeungwa mkono kwa kura 34 kati ya 41.

Kwa mujibu wa ratiba mpya, nchi hiyo changa zaidi duniani itachagua viongozi katika uchaguzi mkuu wa kwanza kabisa Desemba 22, 2026, mwishoni mwa kipindi cha mpito.

Gituai amesisitiza kuwa wakati nchi hiyo inapojiandaa kwa uchaguzi, kukabiliana na hali mbaya ya kiuchumi, ambayo inaendelea kuathiri maisha ya watu wa Sudan Kusini, ni kipaumbele cha kwanza, wakati mafunzo, umoja na kusambaza vikosi muhimu vya umoja pia ni muhimu.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha