超碰caoporen国产公开,亚洲男人在线天堂2019香蕉,国产精品对白刺激,九九热这里只有国产中文精品2

Waziri wa Uganda apongeza juhudi za China katika kulinda mazingira

(CRI Online) Agosti 09, 2024

Waziri wa Mambo ya Ndani wa Uganda Victoria Rusoke Businge amepongeza mchango wa serikali ya China na shirika lisilo la kiserikali la China katika kulinda mazingira na kurejesha misitu nchini Uganda.

Businge aliyasema hayo Jumatano mjini Kampala, wakati akilikabidhi Shirika la Mamlaka ya Kanda ya Ziwa Victoria (LVRLAC) miti na miche ya matunda elfu kumi iliyotolewa na Shirika Liliso la Kiserikali la Mfuko wa Kuokoa Wanyama na Mimea (SWF).

Pia amesisitiza ushirikiano wa muda mrefu kati ya serikali za miji, ikiwa ni pamoja na mji wa Entebbe nchini Uganda, na mji wa Wuhan nchini China kwenye sekta za ujenzi wa miundombinu na uungaji mkono wa mazingira.

Konsuli wa uchumi na biashara katika ubalozi wa wa China nchini Uganda Wang Jianxun amesema China imeanza safari mpya ya kujenga nchi ya ujamaa yenye mambo ya kisasa, ikiwa ni pamoja na uhifadhi wa mazingira, na kuhamasisha kampuni nyingi zaidi za China kushiriki kwenye programu za uhifadhi wa mazingira na majukumu ya kijamii.

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Renato Lu)

Picha