超碰caoporen国产公开,亚洲男人在线天堂2019香蕉,国产精品对白刺激,九九热这里只有国产中文精品2

Masoud Pezeshkian aapishwa kuwa?Rais wa?Iran

(Tovuti ya Gazeti la Umma) Julai 31, 2024

Masoud Pezeshkian (katikati) akiwasili kwenye hafla ya kuapishwa kwake katika bunge mjini Tehran, Iran, Julai 30, 2024. (Xinhua/Shadati)

Masoud Pezeshkian (katikati) akiwasili kwenye hafla ya kuapishwa kwake katika bunge mjini Tehran, Iran, Julai 30, 2024. (Xinhua/Shadati)

TEHRAN - Masoud Pezeshkian ameapishwa kuwa rais wa awamu ya tisa wa Iran siku ya Jumanne katika hafla iliyofanyika kwenye bunge mjini Tehran, ambapo maofisa wa ngazi za juu, makamanda wa kijeshi na wawakilishi kutoka nchi 88 na mashirika 10 ya kimataifa wameshiriki kwenye hafla hiyo, shirika la habari la Iran, IRNA limeripoti.

Kufuatia kiapo chake hicho mbele ya bunge, Pezeshkian ameelezea malengo ya utawala wake, akijikita katika maendeleo ya kiuchumi, maslahi ya taifa na kuboresha maisha ya watu wa Iran.

Amezungumzia malengo muhimu ya sera ya mambo ya nje ya nchi hiyo yenye lengo la kulinda usalama wa taifa na kuimarisha ustawi wa kiuchumi ndani ya mfumokazi wa "heshima, hekima na manufaa."

Pezeshkian pia amelaani vitendo vya Israel huko Gaza, akikosoa mashambulizi ya makombora dhidi ya raia, wakiwemo wanawake na watoto, na wale wanaounga mkono vitendo hivyo.

Pezeshkian mwenye umri wa miaka 69, aliibuka mshindi katika uchaguzi wa urais wa nchi hiyo uliofanyika Julai 6 na akaidhinishwa rasmi na Kiongozi Mkuu wa Iran Ali Khamenei kuwa rais wa awamu ya tisa wa Iran siku ya Jumapili.

Sasa ana siku 15 za kuwasilisha baraza lake la mawaziri bungeni ili kuidhinishwa.

Masoud Pezeshkian akitoa hotuba baada ya kuapishwa kuwa rais wa awamu ya tisa wa Iran kwenye hafla iliyofanyika katika bunge mjini Tehran, Iran, Julai 30, 2024. (Xinhua/Shadati)

Masoud Pezeshkian akitoa hotuba baada ya kuapishwa kuwa rais wa awamu ya tisa wa Iran kwenye hafla iliyofanyika katika bunge mjini Tehran, Iran, Julai 30, 2024. (Xinhua/Shadati)

Masoud Pezeshkian (Mbele) akitoa hotuba baada ya kuapishwa kuwa rais wa awamu ya tisa wa Iran kwenye hafla iliyofanyika katika bunge mjini Tehran, Iran, Julai 30, 2024. (Xinhua/Shadati)

Masoud Pezeshkian (Mbele) akitoa hotuba baada ya kuapishwa kuwa rais wa awamu ya tisa wa Iran kwenye hafla iliyofanyika katika bunge mjini Tehran, Iran, Julai 30, 2024. (Xinhua/Shadati)

Masoud Pezeshkian (Katikati) akipunga mkono wakati akitoka kwenye hafla ya kuapishwa kwake iliyofanyika katika bunge mjini Tehran, Iran, Julai 30, 2024. (Xinhua/Shadati)

Masoud Pezeshkian (Katikati) akipunga mkono wakati akitoka kwenye hafla ya kuapishwa kwake iliyofanyika katika bunge mjini Tehran, Iran, Julai 30, 2024. (Xinhua/Shadati)

Picha iliyopigwa Julai 30, 2024 ikionyesha hafla ya kuapishwa rais katika bunge mjini Tehran, Iran. (Xinhua/Shadati)

Picha iliyopigwa Julai 30, 2024 ikionyesha hafla ya kuapishwa rais katika bunge mjini Tehran, Iran. (Xinhua/Shadati)

Masoud Pezeshkian (Katikati) akiondoka baada ya kutoa hotuba yake ya kuapishwa kuwa rais katika bunge mjini Tehran, Iran, Julai 30, 2024. (Xinhua/Shadati)

Masoud Pezeshkian (Katikati) akiondoka baada ya kutoa hotuba yake ya kuapishwa kuwa rais katika bunge mjini Tehran, Iran, Julai 30, 2024. (Xinhua/Shadati)

(Wahariri wa tovuti:Zhou Linjia,Zhao Jian)

Picha